Popular Posts

Thursday, February 17, 2011

MPANGO SHIRIKISHI WA KUELISHA JAMII BARABARA YA CHALINZE SEGERA TANGA

Wakala wa Barabara Tanzania - TANROADS kwa kushirikiana na Chama cha Malezi Bora Tanzania (UMATI) wapo kwenye zoezi la kuwaelimisha watu waishio kandokando ya barabara ya Chalinze Segera Tanga. Kwa kuanzia katika Mkoa wa Pwani Vijiji kumi na Tatu vitafaidika na mpango huu, Vijiji hivyo ni pamoja na; Bwilingu (Chalinze), Msoga, Mboga, Lunga (Lugoba), Saleni, Mazizi, Msata, Lupungwi, Mandera, Kihangaiko, Kimange, Mbwewe na Kwang'andu.

Timu ya wataalamu wa masuala ya Mazingira, Usalama barabarani, Ukimwi na Nyenzo za Kati za Usafiri wameshaanza zoezi hilo na sasa wapo kijiji cha Saleni na tayari wameshafanya zoezi hilo kwenye vijiji vya Bwilingu, Msoga, Mboga, Lunga na Saleni. Taarifa zaidi zitakuwa zinatolewa siku hadi siku.

No comments:

Post a Comment