Ni jambo lisilo pingika kuwa Bendi ya Twanga Pepeta ni mahali ambapo wasanii wengi wa TASNIA ya muziki huwa wanalilia kwenda. Jambo ambalo limenishangaza na kunistua ni kuondoka kwa Wanamuziki Saba na baadaye mmoja kuamua kurejea kwenye bendi siku mbili tu baada ya kutangazwa na Mkurugenzi wa Bendi hiyo Kamalade Ally Choki.
Wanamuziki walioripotiwa kuondoka ni pamoja na Saulo Fargason, Rogat Hegga Catapiller, Nyamwela, Danger Boy, Otilia Boniphace, Hosea Bass na George Kanuti ambaye amerejea tena kwenye Bendi yake. Habari zinadai kuwa bado Mkurugenzi wa Extra Bongo anakusudia kuwachukuwa wanamuziki wengine ili kuimarisha Bendi yake.
Ikumbukwe kuwa bendi ya Extra Bongo ilishakuwepo kwa kipindi fulani na baadaye kuvunjika miaka michache iliyopita. Sasa najiuliza ni sababu gani zinazopelekea kwa wanamuziki hawa kuondoka kwenye bendi ya Twanga Pepeta. Je? Ni suala la Maslahi kama wanavyodai? La hasha naingiwa na wasiwasi kwakuwa wanamuziki wawili toka Bendi ya Extra Bongo ambao najua wazi kuwa uwezo wao ni Mkubwa wamerejea Twanga Pepeta, sasa kama Bendi hii haina maslahi mbona hawa wamekimbia huko kwenye maslahi. Wadau wa muziki ninaomba maoni yenu juu ya suala hili.
Wanamuziki walioripotiwa kuondoka ni pamoja na Saulo Fargason, Rogat Hegga Catapiller, Nyamwela, Danger Boy, Otilia Boniphace, Hosea Bass na George Kanuti ambaye amerejea tena kwenye Bendi yake. Habari zinadai kuwa bado Mkurugenzi wa Extra Bongo anakusudia kuwachukuwa wanamuziki wengine ili kuimarisha Bendi yake.
Ikumbukwe kuwa bendi ya Extra Bongo ilishakuwepo kwa kipindi fulani na baadaye kuvunjika miaka michache iliyopita. Sasa najiuliza ni sababu gani zinazopelekea kwa wanamuziki hawa kuondoka kwenye bendi ya Twanga Pepeta. Je? Ni suala la Maslahi kama wanavyodai? La hasha naingiwa na wasiwasi kwakuwa wanamuziki wawili toka Bendi ya Extra Bongo ambao najua wazi kuwa uwezo wao ni Mkubwa wamerejea Twanga Pepeta, sasa kama Bendi hii haina maslahi mbona hawa wamekimbia huko kwenye maslahi. Wadau wa muziki ninaomba maoni yenu juu ya suala hili.
No comments:
Post a Comment